KARIBU KATIKA BLOG HII YA KIFALME. KWA MAWASILIANO: +255715006977

Thursday, April 7, 2011

FILAMU MPYA YA JB HIYOOO...

FILAMU mpya iliyotokea kujizolea umaarufu mkubwa kabla haijatoka, inayokwenda kwa jina la ‘Senior Bachelor’, inatarajiwa kutinga sokoni Jumatatu, Aprili 18, mwaka huu ambako itapatikana kwenye mikanda ya kawaida, VHS, VCD pamoja na DVD.
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Jerusalem Film Company, Jacob Stephen ‘JB’ alimweleza mwandishi wa habari hizi jijini Dar es Salaam jana kuwa, filamu hiyo imebeba ujumbe mzito kwa jamii kwa kuanika upande wa pili wa maisha ya Mapedeshee.
“Unajua, filamu yangu hii mpya imewamulika Mapedeshee na maisha yao kwa ujumla, kwani wengi wao hupenda kuonyesha ufahari na kumwaga pesa kwenye majumba ya starehe, wakati kumbe hata pa kulala hawana na mwishowe hutokea kujikuta wakifia katika nyumba za wageni,” alisema JB.
Aidha, JB alisema, katika filamu hiyo ya pili kutolewa na Kampuni yake kwa mwaka huu, amecheza yeye mwenyewe pamoja na nyota wengine kadhaa wa maigizo kama Jack wa Chuzi, Jackline Uwoya na mkongwe wa muziki kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Bozi Boziana.

No comments:

Post a Comment