KAMPUNI inayojihusisha na ukuzaji vipaji vya wasanii nchini, Twins Art Production keshokutwa Jumatatu inatarajia kufungua Studio ya kurekodia muziki itakayojulikana kama ‘Twins Records’.
Meneja Mkuu wa Twins Art, Daud Juma Mwandalima aliiambia Blog hii jijini Dar es Salaam jana kuwa, Studio hiyo itakuwa ikirekodi kazi mbalimbali za wasanii wa muziki.
Aidha, Mwandalima alieleza kuwa, Studio hiyo ambayo Mkurugenzi Mkuu wake ni Vick Kanyoka, itakuwa vilevile ikiandaa matamasha pamoja na kuwasaidia wasanii walio katika mazingira magumu.
“Pia tutakuwa na kikundi cha wasanii mahiri ambao kazi yao itakuwa ni kurekodi matangazo ya kibiashara kwenye Kampuni mbalimbali tutakazokubaliana nazo, ndani na nje ya nchi,” alisema Mwandalima.
No comments:
Post a Comment